Kwenye mechi za kombe la ligi zilizofanyika jana nchini Uingereza, Manchester United imeondolewa kwenye mashindano hayo kwa njia ya penati 7-8 baada ya kupata sare ya 2-2 kwenye muda wa kawaida na Derby County.
Licha ya United kuonyesha uhai kwenye dakika za lala salama za mechi hiyo, bado haikusaidia kwani waliambulia goli la kusawazisha lililofungwa na Maroune Fellaine kunako dakika ya 95.
Katika mechi zingine zilizopigwa jana, matokeo yalikuwa kama ifuatavyo.
AFC Bournemouth 3 - 2 Blackburn Rovers
Blackpool 2 - 0 Queens Park Rangers
Burton Albion 2 - 1 Burnley
Millwall 1 - 3 Fulham
Oxford United 0 - 3 Manchester City
Preston North End 2 - 2 Middlesbrough *
Wolverhampton Wanderers 0 - 0 Leicester City *
Wycombe Wanderers 3 - 4 Norwich City
Manchester United 2 - 2 Derby County *
West Bromwich Albion 0 - 3 Crystal Palace
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |