Kikosi cha timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars kinatakiwa kusafiri hadi mji wa Bahir Dar Oktoba 10 kukabiliana na Ethiopia kisha timu hizo mbili zirudiane siku tatu baadaye, Oktoba 14 katika uga wa MISC Kasarani nchini Kenya.
Shirikisho la soka nchini(FKF) lilikuwa limekadiria bajeti ya shilingi milioni 26 kugharamia mikondo miwili ya mechi hiyo lakini hadi sasa FKF haijapokea mawasiliano yoyote au ithibati kutoka wizara ya michezo kwamba pesa hizo zitatolewa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |