Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Rwanda (Amavubi) Vicent Mashami ameshatangaza orodha ya wachezaji ambao anawataka kambini kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi dhidi ya Guinea ya kusaka tiketi ya kushiriki AFCON 2019 nchini Cameroon. .
Mechi hiyo itapigwa mnamo Oktoba 12 nchini Guinea na kurudiwa Oktoba 16 nchini Kenya. kwenye makao ya FERWAFA, kocha huyo amewatangaza majina ya wachezaji 27 atakaowatumia.
Kocha huyo ameongeza wachezaji wapya wawili kwenye timu hiyo huku akiwa na matumaini ya timu yake kukata tiketi ya kufuzu michuano hiyo licha ya kupoteza mechi mbioli mfululizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |