• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Israel kufungua tena kivuko cha milima ya Golan

    (GMT+08:00) 2018-09-28 09:11:13

    Waziri wa ulinzi wa Israel Bw. Avigdor Lieberman amesema Israel iko tayari kufungua tena kivuko cha mpaka na Syria huko Quneitra katika milima ya Golan, sehemu inayotenganisha Israel na Syria.

    Amesema hayo akizungumza na wanahabari katika kivuko cha Quneitra upande wa Israel. Amesema hali ya usalama katika eneo la Quneitra imeanza kuboreshwa, kikosi cha waangalizi wa Umoja wa Mataifa walioko katika eneo hilo la kutenganisha Israel na Syria kimerejea katika kivuko cha Quneitra na kusubiri kufunguliwa tena.

    Amesisitiza tena kwamba Israel haina madhumuni ya kuingilia mambo ya ndani ya Syria.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako