Kampuni ya kimataifa ya fedha inayomilikiwa na benki ya dunia IFC imewekeza jumla ya shilingi bilioni 20 nchini Kenya hadi mwezi wa juni mwaka huu na inatarajia kiwango hicho kuongezeka mara mbili ifikapo juni mwaka ujao. Kampuni hiyo imesema inaratajia kuwekeza jumla ya shilingi bilioni 100 pekee nchini Kenya kwenye mpango wake wa uwekezaji. Akizungumza mjini Nairobi, mkurugenzi wa IFC
Oumar Seydi amesema kampuni hiyo ina mpango wa uwekezaji wa muda mrefu na miongoni mwa makampuni ambayo wamewekeza ni pamoja na Goodlife Pharmacies na taasisi zingine za fedha.Kampuni hiyo pia imeonyesha nia ya kuwekeza kwenye kampuni ya Athi River Mining ili kuzuia isisambaratike.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |