Maendeleo yamepatikana katika majadiliano kati ya mamlaka za Syria na wapiganaji wa kundi la IS, kuhusu kukamatwa kwa mateka kutoka mkoa wa Sweida, kusini mwa Syria.
Shirika la Uangalizi wa Haki za Binadamu la Syria, limesema makubaliano ya mwisho yanaweza kufikiwa ndani ya muda mfupi, na kuongeza kuwa kundi la IS linaweza kuwaachia huru mateka hao kama mamlaka za Syria zikikubali kuwaruhusu wapiganaji wake waliobaki, kuondoka milima ya Tulol al-Safa, eneo la mwisho linalodhibitiwa na IS katika sehemu za pembezoni mashariki mwa mkoa wa Sweida.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |