Vyama vya Wafanyakazi nchini Nigeria vimetangaza kusimamisha mgomo kote nchini ulioanza Alhamisi kwa ajili ya kupinga serikali kushindwa kujibu madai yao ya kuongezwa kwa kima cha chini cha mshahara ndani ya siku 14.
Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi la Nigeria Bw. Ayuba Wabba amesema mgomo huo umesimamishwa mara moja ili kuiwezesha serikali kuandaa mkutano muhimu na kufanya maamuzi kuhusu kima cha chini cha mshahara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |