• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kikapu, Wanawake: Ubingwa wa dunia ngazi ya Kanda Afrika Mashariki

    (GMT+08:00) 2018-10-02 10:11:13

    Timu ya Mamlaka ya Bandari ya Kenya KPA ya mchezo wa mpira wa kikapu ya wanawake jana imefanikiwa kupata ushindi wa 50-49 kwenye mechi yake ya kwanza dhidi ya timu ya APR kutoka Rwanda katika mashindano ya ubingwa wa kanda ya Afrika mashariki yanayoendelea mjini Dar es Salaam nchini Tanzania.

    Katika mechi zingine zilizopigwa jana, Patriots ya Rwanda iliishinda Wolkite ya Ethiopia kwa alama 84-34 na JKT ya Tanzania ikishinda kwa alama 88-81 dhidi ya Cobra ya Sudan Kusini.

    Aidha Strathmore kutoka Kenya ilipita bila kupingwa baada ya wapinzani wake New Star ya Burundi kushindwa kufika uwanjani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako