Rais Mulatu Teshome wa Ethiopia amesema mafanikio ya ajenda ya maendeleo endelevu yanataka mageuzi ya data ili kuunga mkono mipango ya maendeleo ya bara la Afrika katika ngazi zote.
Rais Teshome amesema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 6 wa Kamati ya Takwimu ya Afrika uliofanyika jana mjini Addis Ababa, Ethiopia. Amesema mageuzi ya data yanaboresha uvumbuzi na teknolojia katika ngazi zote za mchakato wa takwimu kama kukusanya, kutathmini na kupambanua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |