Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Mike Pompeo amesema anatumai kuwa mazungumzo yajayo na Korea Kaskazini yatafikia maelewano mapana na maendeleo makubwa zaidi.
Akiongea na wanahabari, Bw. Pompeo amesema kwenye mazungumzo yajayo, Marekani na Korea Kaskazini zinatarajiwa kuweka mpango wa kuendeleza juhudi za kuondoa silaha za nyuklia kwenye peninsula ya Korea, na vikwazo vya Marekani dhidi ya Korea Kaskazini vitaendelea kutekelezwa.
Imefahamika kuwa Bw. Pompeo atakwenda Korea Kaskazini na kukutana na kiongozi wa nchi hiyo Bw. Kim Jong Un Jumapili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |