Klabu ya Simba Sports ya Tanzania inajulikana Zaidi kama wekundu wa msimbazi imeanza ujenzi wa uwanja wake wa kisasa katika eneo la Bunju jijini Dar es salaam chini ya bilionea kijana Mohamed Dewji "Mo".
Mo Dewji ambaye yuko mbioni kununua asilimia 49 ya hisa za klabu hiyo, amesema anatarajia zoezi hilo lililoanza jana litakamilika kabla ya Februari 2 mwakani, na kusema huu ni wakati wa historia kwa klabu hiyo kwakuwa imechelewa sana kuwa na kiwanja chake binafsi licha ya kuwa moja ya timu kubwa Afrika.
Jana waandishi walishuhudia magreda yakianza kazi katika uwanja huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |