Licha ya majina makubwa Geoffrey Kirui, Dickson Chumba na Abel Kirui kutoka Kenya kuwa katika orodha ya washiriki watakaotimka katika mashindano yam bio ya Chicago (Chicago Marathon) hapo Oktoba 7, mwaka huu, vita vya taji vimetabiriwa vitakuwa vikali kati ya Mwamerika Galen Rupp na Muingereza Mo Farah.
Wakenya Bernard Kipyego na Kenneth Kipkemoi pia watashiriki mashindano hayo ya 41, ambayo yamevutia washiriki 45, 000 kutoka zaidi ya mataifa 100 duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |