Shindano la kila mwaka la Balozi wa Korea ambalo huandaliwa na shirikisho la mchezo wa Taekwondo nchini Rwanda kushirikiana na Balozi wa Korea nchini humo linatarajiwa kuanza kesho Oktoba 6 na 7 ikiwa ni mara ya sita tangu kuanzishwa kwake.
Rais wa shirikisho la mchezo huo nchini Rwanda Placide Bagabo amesema timu 29 toka nchi mbalimbali toka Afrika Mashariki zimethibitisha kushiriki ikiwemo wenyeji Rwanda, Kenya, Tanzania, Uganda, D.R.C, Burundi, na Sudan.
Pia mwaka huu itakuwa mara ya kwanza kwa watu wenye ulemavu kushiriki katika shindano hilo lijulikanalo kama Para-Taekwondo
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |