Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea jana kupigwa kwenye viwanja tofauti. Matokeo ya mechi za makundi yenye msisimko na ushindani Kundi B: Celtic imekubali kipigo cha 3-1 toka kwa Salzburg na katika kundi E: Arsenal ameibuka na ushindi mnono wa goli 3-0 dhidi ya Qarabag FK, nayo AC Milan imeifunga Olimpiacos goli 3-1 katika mchezo wa kundi F, Villarreal imelazimishwa sare ya 3-3 na Spartak Moscow katika kundi G,nayo Appolon Limassol imeilazimisha Marseille suluhu ya 2-2 katika mchezo wa kundi H, huku Sarposborg 08 ikiibamiza Genk kwa bao 3-1 katika kundi I, FC Krasnodar ikiizamisha Sevilla kwa goli 2-1 kundi J. nayo Chelsea fc imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Vidi fc katika kundi L
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |