Mtu mmoja amefariki, mwingine kujeruhiwa, na nyumba 60 kuharibika baada ya lori la mafuta kulipuka katika mji wa kibiashara wa Duala, nchini Cameroon mapema leo.
Chanzo cha habari kutoka jeshi la polisi kimeliambia Shirika la Habari la China Xinhua kuwa, mazingira yaliyosababisha mlipuko huo bado hayafahamiki, lakini lori hilo lilikuwa limebeba takataka kutoka kampuni moja ya Ufaransa nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |