Tanzania imezuia mjadala kuhusu muswada wa kuwa na sheria moja ya takwimu katika jumuiya ya Afrika Mashariki uliopendekezwa na wabunge wa bunge la Afrika Mashariki EALA.
Waziri wa masuala ya Afrika Mashariki kutoka Burundi Isabelle Ndahayo alitangaza kuahirishwa kwa majadiliano kuhusu muswada huo kufuatia ombi la Tanzania.
Wabunge 13 wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda na Sudan Kusini waliunga mkono penedekezo la kuahirishwa mjadala huo.
Tanzania imeomba kupewa muda zaidi wa mpitio na mashauriano kuhusu muswada huo ambao unalenga pia kuanzia idara ya kusimamia takwimu kikanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |