Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema maeneo ambayo bado yanakaliwa na waasi nchini humo yatarudi katika udhibiti wa serikali, na kuongeza kuwa makubaliano ya eneo lisilo na shughuli za kijeshi katika mkoa wa Idlib ni ya muda.
Uturuki na Russia zimekubaliana kuanzisha eneo lisilo na shughuli za kijeshi kaskazini magharibi mwa Syria kabla ya tarehe 15 Oktoba kati ya jeshi la serikali ya Syria na waasi, ambao wanatakiwa kuondoa silaha nzito kutoka eneo hilo litakalofanyiwa doria na vikosi vya Uturuki na Russia. Jeshi la serikali pia lilipanga kufanya shambulizi ili kutwaa tena udhibiti wa mkoa wa Idlib na maeneo mengine yanayodhibitiwa na waasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |