Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Kazi kwa Wakimbizi wa Palestina UNRWA limekosoa mauaji ya wakimbizi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza mashariki, na pia kueleza kuhuzunishwa na msukosuko wa kibinadamu unaokithiri katika eneo hilo. UNRWA imesema kwenye taarifa yake kuwa tarehe 28, Septemba vurugu huko Gaza zilisababisha vifo vya wapalestina saba wakiwemo watoto wawili, mmoja wao ni mwanafunzi wa shirika hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |