Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema watu zaidi ya laki 1.9 waliopoteza makazi yao nchini Libya wanahitaji msaada zaidi.
Shirika hilo limetoa taarifa ikisema wakimbizi hao wanahitaji misaada zaidi ili kuweza kurudi nyumbani hali ikiruhusu.
Taarifa pia imesema shirika hilo litaendelea kuunga mkono na kutoa misaada kwa wakimbizi, kwa kutoa bidhaa zisizo za chakula, fedha na kutekeleza miradi itakayotimizwa kwa haraka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |