• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Afrika Kusini asisitiza umuhimu wa mageuzi ya ardhi katika kutimiza amani nchini humo

    (GMT+08:00) 2018-10-09 10:10:00
    Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amesema, nchi hiyo haitatimiza amani halisi kabla ya kutatua suala la ardhi.

    Akihutubia mkutano wa 8 wa maadhimisho ya Desmond Tutu uliofanyika mjini Cape Town, Bw. Ramaphosa amesema, amani sio tu kutokuwepo vita, bali pia ni kutokuwepo hali isiyo na haki. Pia amehimiza kuunga mkono mageuzi mapya ya kutwaa ardhi bila fidia.

    Bw. Ramaphosa amesema, ni lazima wajenge nchi ambayo fedha ziwe mali ya wananchi na ardhi idhibitiwe na wanaoitolea jasho, ili kutimiza amani endelevu nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako