Kampuni ya kitaifa ya mafuta ya Uganda imepata kipande cha ardhi cha ekari 300 katika wilaya ya Wakiso ambapo itajenga hifadhi ya mafuta.
Hifadhi hiyo itakuwa na uwezo wa kuhifadhi lita milioni 60 za bidhaa za petroli.
Mkuu wa fedha kwenye kampuni hiyo Emmanuel Mugagga, amesema wanatafuta mshirika wa kujenga hifadhi hiyo inayotarajiwa kugharimu dola milioni 51.
Hifadhi hiyo itatumika kama kituo cha kugawa bidhaa za petroli ambazo zitatokea kwenye kiwanda cha usafishaji wa bidhaa hiyo katika wilaya wa Hoima.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |