Maofisa waandamizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika jana walisema hali ya vurugu nchini Sudan Kusini imepungua kuliko mwaka jana, baada ya kusaini makubaliano ya amani kati ya makundi yanayopigana mwezi Agosti.
Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia operesheni za ulinzi wa amani Bw. Jean Pierre Lacroix, amesema maofisa hao wamefurahi kuona pande hasimu zimepata maendeleo, hasa katika kukomesha mapambano katika majimbo ya Yei River na Unity.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |