Rais Xi Jinping wa China ametoa wito wa kufanyika juhudi za kuongeza uwezo wa kulinda usalama katika kukabiliana na maafa ya kimaumbile, na kuzindua rasmi mipango na ujenzi wa reli inayounganisha mikoa ya Sichuan na Tibet. Amesema uwezo huo unahusu uchumi na maisha ya watu, na China itazindua mfumo wenye ufanisi na wa kisayansi na kuongeza uwezo wa jamii nzima katika kulinda maisha na mali za watu na usalama wa taifa. Pia amesisitiza kuwa reli ya kutoka Sichuan hadi Tibet ina umuhimu mkubwa kwa ajili ya utulivu wa muda mrefu wa nchi na maendeleo ya Tibet.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |