• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RIADHA: Mwanariadha wa Kenya apigwa nyundo ya miaka minne

    (GMT+08:00) 2018-10-11 09:00:13
    Mwanariadha wa Kenya Samuel Kalalei amefungiwa kushirikia michuano ya riadha kwa kipindi cha miaka minne baada ya matokeo ya vipimo vyake vya damu kuchunguza kama alikuwa akitumia dawa za kusisimua misuli.

    Kitengo cha kuzuia matumizi ya dawa za kuongeza nguvu na kusisimua misuli michezoni (AIU) kimesema, Kalalei mwenye umri wa miaka 23 alifanyiwa vipimo wakati wa michuano ya riadha ya Rotterdam mwezi April ambapo alimaliza mashindano hayo kwa kukamata nafasi ya 7.

    Wanariadha wa Kenya wamekuwa wakikumbwa na rungu hilo miaka ya karibuni, akiwemo mwanariadha aliyeshinda medali katika mashindano ya Rio Olimpiki yam waka 2016, Jemima Sumsong.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako