• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Michuano ya kufuzu AFCON 2019, Stars yatua Cape Verde, Museveni awamwagia mapesa the Cranes, Kenya na Ethiopia hakuna mbabe

    (GMT+08:00) 2018-10-11 09:01:33

    Timu ya soka ya Tanzania (Taifa Stars) imewasili na kuanza mazoezi jana jioni katika uwanja wa taifa wa Praia jiji la Praia nchini Cape Verde kujiandaa na pambano lake dhidi ya timu ya taifa ya Cape Verde kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani yatakayofanyika nchini Cameroon.

    Tayari mastaa wa timu hiyo wanaocheza soka la kulipwa Mbwana Samatta anayekipiga Genk ya Ubelgiji na Simon Msuva anayecheza klabu ya Jadida ya Morocco wameshaungana na taifa stars.

    Nae rais wa Uganda Yoweri Museveni jana usiku amekutakana na kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo (Uganda the Cranes) ikiwa inajiandaa kwa safari ya kuifuata Lesotho kwa mchezo wa marudiano wa kufuzu michuano hiyo.

    Museveni ametoa shilingi milioni 5 za Uganda kwa kila mchezaji, na shilingi milioni 200 kwa timu nzima kama motisha ili timu hiyo ipate ushindi.

    Timu nyingine ya Afrika Mashariki, Harambee Stars ya Kenya imelazimishwa sare ya bila kufungana na timu ya taifa ya Ethiopia katika mchezo uliochezwa jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako