Baraza la mawaziri la Kenya limepitisha uamuzi wa kuanzishwa kwa Baraza la Mamlaka za Barabara za Kikanda EARRAF, ikiwa ni juhudi za kuratibu miundombinu ya barabara katika Afrika Mashariki, haswa katika barabara zinazovuka mipaka ya nchi katika ubunifu, vigezo na gharama. Ikulu ya Kenya imesema EARRAF itaratibu kazi za mashirika mbalimbali katika kutekeleza na kusimamia miundombinu ya barabara katika kanda hiyo, na bodi za usimamizi wa barabara za Kenya, Uganda na Tanzania zitahusishwa pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |