Mo alitekwa jana asubuhi wakati akielekea kufanya mazoezi ya viungo (gym) katika hoteli ya Colosseum iliyopo jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema Mo ametekwa na raia wawili wa kigeni.
Kwa upande wa klabu ya Simba kupitia kwa msemaji wake Haji Manara, imewataka wanachama na mashabiki wake kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho vyombo vya dola vinafanya jitihada kuhakikisha Mo anapatikana akiwa salama.
Nayo klabu ya Yanga imesema ukiachana na masuala ya utani wa jadi, imeguswa na kusikitishwa na taarifa za kutekwa kwa Mo ambaye ni mtu muhimu kwa watani wao Simba pamoja na mpira wa Tanzania, hivyo inamuombea kheri huko aliko na apatikane akiwa salama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |