• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda kuandaa mkutano wa Jumuiya ya Madola

    (GMT+08:00) 2018-10-12 08:33:47
    Shirikisho la michezo ya jumuiya ya madola (CGF) limeitangaza Rwanda kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa shirikisho hilo utakaofanyikwa nchini humo Septemba 4 hadi 8 mwakani.

    Rais wa CGF Louise Martin ameelea kuwa uanachama wa Rwanda katika Jumuiya ya madola ni wa aina yake na kwakuwa Rwanda itakuwa inatimiza miaka 10 tangu kujiunga na jumuiya hiyo, wanataka kutumia nafasi hiyo kujenga jina la Rwanda katika michezo hiyo.

    Mkutano huo utafanyika mjini Kigali ambapo agenda kubwa itakuwa Uchaguzi Mkuu wa CGF kupitia sheria zinazoongoza shirikisho hilo na kanuni zake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako