Polisi wa Uganda wametuma vikosi vya uokoaji kwenye wilaya ya Bududa, mashariki mwa nchi hiyo, ambako makumi ya watu wamefariki dunia kutokana na maporomoko ya ardhi.
Msemaji wa polisi ya wilaya ya Elgon, Bw. Sowed Mansur amesema, kikosi cha kwanza cha uokoaji kimepata miili 17. Lakini kazi ya uokoaji ilisimama wakati wa usiku kutokana na giza. Bw. Mansur ameahidi kuwa leo kikosi hicho kitaendelea na kazi ya uokoaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |