Mchungaji Andrew Brunson ambaye Marekani aliondoka jana nchini Uturuki kwa ndege binafsi saa chache baada ya mahakama nchini humo kuamuru kuachiliwa kwake akiwa tayari ametumikia sehemu ya kifungo cha miaka 3, mwezi mmoja na siku 15 kutokana na tuhuma zinazohusiana na ugaidi.
Brunson amabye alihukumiwa kwenda jela nchini Uturuki mwezi Disemba mwaka 2016 aliondoka jana usiku katika uwanja wa ndege wa Adnan Menderes na kuelekea nchini Ujerumani ambako atakaa kwa siku mbili kabla ya kuanza safari ya kwenda Marekani.
Kuachiliwa kwa Brunson kumepunguza mvutano uliojitokeza kati ya Uturuki na Marekani uliopelekea Marekani kuiwekea vikwazo vya kibiashara Uturuki mwezi Agosti mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |