Wizara ya mambo ya nje ya Syria imetoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi wa kimataifa dhidi ya vitendo vya uhalifu dhidi ya muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani kufuatia shambulizi la hivi karibuni lililotumia roketi ya Phosphorus dhidi ya mkoa wa Deir al-Zour. Imesema matumizi ya silaha zinazopigwa marufuku kimataifa dhidi ya watu wa Syria yamekiuka vikali sheria ya kimataifa na haki za binadamu. Pia imetaka kumaliza uwepo wa kivamizi na haramu wa vikosi vya Marekani nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |