Felician Muhitira wa Rwanda ameshinda medali ya fedha kuwa kushika nafasi ya pili kwenye mbio za kilomita 20 za mjini Paris nchini Ufaransa.
Muhitira alitumia dakika 58 na sekunde 35 katika mbio hizo, na nafasi ya kwanza ilikamatwa na Samuel Tsegay kutoka Eritrea aliyetumia dakika 58 na sekunde 23.
Nafasi ya tatu katika mbio hizo ilikwenda kwa Hassan Chahdi wa Ufaransa aliyetumia dakika 59, na sekunde 51.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |