Jeshi la Somalia limepambana na wapiganaji wa Kundi la al-Shabab kusini mwa Somalia, na kuwaua wapiganaji wasiopungua wanane na kuwajeruhi wengine kadhaa.
Kamanda wa divisheni ya 60 ya jeshi la Somalia Bw Ismail Khalif Shire amesema asakri mmoja aliuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa kwenye mapambano hayo yaliyotokea Daynunay, kilomita 30 mashariki mwa mji wa Baidoa.
Bw. Shire amesema jeshi lake limewaua wapiganaji wanane wa Kundi la al-Shabab na kuwajeruhi wengine kadhaa, ambapo limevunja ndoto yao ya kutwaa eneo hilo. Wapiganaji wa Kundi la al-Shabab wamedai kuwa wamedhibiti eneo la Daynunay na kukamata silaha kutoka kituo cha jeshi kwenye eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |