China imetangaza mpango wa kujenga eneo la majaribio la biashara huria katika kisiwa cha Hainan kilichoko kusini mwa nchi hiyo.
Mpango huo uliotolewa na Baraza la Serikali la China umeelekeza kuwa, katika kujenga eneo hilo, ambalo ni hatua kubwa inayodhihirisha utayari wa China wa kufungua mlango zaidi na kuendeleza utandawazi wa kiuchumi duniani, kisiwa hicho kitapata fursa zaidi ya mageuzi na kuongeza kasi ya mazingira rahisi ya kibiashara ya kimataifa na yenye kufuata sheria, pia kuwa na mazingira ya soko la makini, la usawa, la wazi na la pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |