Mjini Dar es Salaam jana, timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imepata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Cape Verde katika mechi ya kufuzu Afcon 2019.
Magoli ya Tanzania yalifungwa na Simon Msuva na Mbwana Samata, na kuifanya timu hiyo ishike nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi L kwa kufikisha alama 5.
Uganda ambayo ilishinda mechi yake ya jana kwa magoli 2-0 dhidi ya Lesotho ndiyo inaongoza kundi L kwa kuwa na alama 10.
Katika kundi hilo, kila timu imebakiza mechi mbili ili kukamilisha mzunguko wa kufuzu, na baada ya hapo timu ya kwanza na timu ya pili kwenye msimamo ndizo zitakazofuzu Afcon 2019.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |