Watu zaidi ya 19, wengi wakiwa ni vijana wameuawa na wengine 40 kujeruhiwa katika shambulizi lililotokea katika chuo cha ufundi stadi mjini Kerch, Crimea. Kwa mujibu wa ripoti, vifaa vya milipuko visivyojuliakana vililipuka katika mgahawa wa chuo kikuu na mlipuko huo uliambatana na ufyatuaji risasi. Ofisi ya Idara ya Uendeshaji Mashtaka ya Ukraine huko Crimea na Kamati ya Uchunguzi ya Russia, kila upande umeanza uchunguzi dhidi ya tukio hilo chini ya tuhuma za vitendo vya kigaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |