China na nchi zaidi ya 10 za Ukanda Mmoja, Njia Moja zimeahidi kujenga ushirikiano wa kiwenzi katika mambo ya nishati ili kuingiza nguvu mpya kwenye maendeleo ya nishati ya nchi mbalimbali.
Ahadi hiyo imetolewa kwenye taarifa ya pamoja iliyotangazwa katika mkutano wa mawaziri wa nishati wa Ukanda Mmoja, Njia Moja uliofanyika mjini Suzhou, mashariki mwa China. Kuhimiza matumizi ya nishati safi, salama na zenye ufanisi kumekuwa ni kazi ya pamoja duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |