Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema limewaondoa wakimbizi wanyonge 135 na watu wanaotafuta hifadhi kutoka Libya hadi Niger, kutokana na kuongezeka kwa hali mbaya ya kiusalama mjini Tripoli. Kwa mujibu wa taarifa, wengi wa wakimbizi hao walikuwa wanashikiliwa kwa miezi kadhaa na kusumbuliwa na utapiamlo na matatizo ya kiafya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |