• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Riadha: Tanzania yaibuka kidedea Nagai Marathon

    (GMT+08:00) 2018-10-22 08:43:23

    Wanariadha kutoka Tanzania wamepata ushindi wa jumla kwenye mbio za Marathon za Nagai zilizofanyika jana nchini Japan baada ya kufanya vyema.

    Katika mbio za kilomita 42 Marco Joseph ameshinda nafasi ya kwanza akifuatiwa na Wilbald Peter ambaye ni kutoka Tanzania.

    Kwa upande wa wanawake Anjelina John wa Tanzania alishinda kwa kutumia saa 2 dakika 43 na sekunde 21.

    Nako kwenye mbio za nusu marathon za kilomita 21 Fabian Nelson wa Tanzania ameshinda nafasi ya kwanza na kwa wanawake nafasi ya kwanza hadi ya nne imetwaliwa na watanzania.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako