Kocha Masoud Juma Irambona wa Burundi amesaini rasmi mkataba wa mwaka mmoja wa kuifundisha klabu ya AS Kigali inyaoshiriki ligi kuu nchini Rwanda.
Tangazo la nafasi hiyo ya kazi lilitolewa wiki moja iliyopita baada ya AS Kigali kuachana na kocha wake wa zamani.
Kuajiriwa kwa Masoud kunafuta tetesi kuwa timu hiyo ilikuwa mbioni kumwajiri kocha wake wa zamani Andre Mbungo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |