Mkutano mkuu wa 17 wa wajumbe wa mashirikisho ya wafanyakazi ya China umefunguliwa leo asubuhi hapa Beijing na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo rais Xi Jinping na waziri mkuu Li Keqiang.
Akizungumza kwa niaba ya Kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China, Mjumbe wa kudumu wa Ofisi ya siasa ya Kamati hiyo Bw. Wang Huning amesema, tangu mkutano mkuu wa 16 wa mashirikisho ya wafanykazi ya China, mashirikisho ya wafanyakazi ya ngazi mbalimbali yamepata maendeleo kwenye kujenga uhusiano wa uwiano katika sehemu za kazi, kuhimiza mageuzi ya timu ya wafanyakazi wa viwanda, na kufanya uvumbuzi wa mashirikisho ya wafanyakazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |