Mradi wa ujenzi na urekebishaji nyumba jijini Nairobi unatarajiwa kuanza mwezi ujao kwa mujibu wa Gavana wa Nairobi Mike Sonko.
Awamu ya kwanza ya mradi huo wa thamani ya shilingi bilioni 300 unatarajiwa kujenga baina ya uniti 10,000 hadi 12 za nyumba.
Nyumba hizo zitarekebishwa na kujenga upya katika maeneo ya Ngara,Pangani na Ngong.
Wapangaji wanaoendelea kuishi katika nyumba za upangaji hawatapandishiwa kodi baada ya marekebisho ya nyumba hizo.
Aidha nyumba mpya zitakazojengwa zitapandishwa kodi na wapangaji wa zamani watalipwa fidia na kuondolewa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |