• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda:Daraja kuu la kuvukia River Nile kujengwa Uganda

    (GMT+08:00) 2018-10-22 20:18:45

    Rais Yoweri Kaguta Museveni amezindua rasmi ujenzi wa daraja la mita 525 litakaloitwa darala la mto Nile katika eneo la Jinja Uganda.

    Daraja hilo la gharama ya dola milioni 112 litajengwa na kampuni ya Japan.

    Kwa mujibu wa wanauchumi,daraja hilo litatumika pakubwa katika kurahisisha uchukuzi wa bidhaa kuingia na kutoka Uganda hadi Kenya jambo litakaloimarisha uchumi.

    Zaidi ya watu 800 watahusika katika ujenzi wa daraja hilo litakalokuwa la pili kwa ukubwa baada ya lile ya Kigamboni la Tanzania.

    Daraja hili pia litatumika kuvutia watalii na wahandisi wanasema, litaweza kudumu kwa kwa zaidi ya miaka 120.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako