Rais Xi Jinping wa China leo amezindua daraja linalounganisha miji ya Hongkong, Zhuhai na Macao mjini Zhuhai, mkoani Guangdong nchini China.
Rais Xi ametembelea daraja hilo na kuwashukuru watu walioshiriki kwenye usanifu, ujenzi, na usimamizi wa daraja hilo mpaka kukamilika kwake.
Rais Xi Jinpiing amewataka watu husika watumie vizuri daraja hilo, ili kuonesha umuhimu mkubwa kwa ujenzi wa eneo la ghuba ya Guangdong, Hongkong na Macao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |