Michezo nane ya UEFA Champions League hatua ya makundi imepigwa usiku wa jana kwenye viwanja mbalimbali. Barcelona imecheza bila ya Lionel Messi imeibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Inter Milan, Monaco ikilazimishwa sare ya 0-0 na Club Brugge, PSV Eindhoven nayo imetoka sare ya 2-2 na Tottenham Hotspur, huku Borussia Dortmund ikiipa kichapo Atletico Madrid, Liverpool imeikandamiza Crvena Zvezda 4-0, Paris Saint Germain (PSG) ikitoka suluhu ya 2-2 na Napoli, nayo Galatasaray na Schalke 04 hazijaonyeshana ubabe baada ya kutoka sare ya bila kufungana, Lokomotiv Moscow imekubali kichapo toka kwa FC Porto.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |