Mamlaka ya kuuza nje kahawa nchini Uganda inaripoti kwamba mauzo ya bidhaa hiyo kwenye soko la kimataifa yameongezeka kwa magunia 300,000 hadi septemba mwaka huu,.
Uganda iliuza magunia milioni 4.8 kati ya Januari na Septemba 2018 ikilinganishwa na magunia milioni 4.5 kipindi sawa na hicho mwaka jana.
Taakwimu za mamlaka hiyo zinaonyesha kuwa mauzo hayo yaliiletea Uganda dola milioni 472.
Mamlaka hiyo inasema ongezeko la mauzo na kahawa yenyewe zimechangiwa na mvua za kutosha .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |