Klabu ya Real Madrid imemfuta kazi kocha wake Julen Lopetegui baada ya miezi minne na nusu ya kudumu katikia klabu hiyo. Mhispania huyo alichukua mikoba kutoka kwa Zidedine Zidane mwezi juni. Huu ni mwanzo mbaya zaidi kwa real madrid tangu msimu wa mwaka 2001-2002.
Mikoba ya Lopetegui sasa itarithishwa na Santiago Solari kocha wa timu ya vijana wa timu hiyo.