Ndege iliyosanifiwa na China ARJ21 imeanza safari zake tatu za ndani.
Shirika la Kutengeneza Ndege la China (COMAC) linalomilikiwa na serikali kuu limesema, shirika la ndege la Chengdu limeanza kutumia ndege hiyo katika safari zake tatu za ndani katika mpangilio wa safari za ndege za majira ya baridi ya mwaka huu na majira ya mchipuko ya mwaka ujao. Safari hizo ni kutoka Chengdu – Hengyang-Quanzhou, Chengdu – Taiyuan – Harbin, na Chengdu – Linfen – Harbin, zikiunganisha mji mkuu wa mkoa wa Sichuan ulioko kusini magharibi mwa China na miji mingine mikuu nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |