Wakala wa Usain Bolt, Ricky Simms alitaka mteja wake apewe mkataba wa Shilingi milioni 213.3, lakini ripoti zinasema klabu hiyo kutoka Ligi Kuu ilikuwa tayari kumpa asilimia tano pekee yaani shilingi milioni 10.6 kwa sababu haikuridhishwa sana na kipaji chake.
Mwanariadha huyu wa rekodi ya mbio za dunia ya amekuwa akifanyiwa majaribio na klabu hiyo tangu awasili mwezi Agosti. Alitumai kutimiza ndoto yake ya utotoni ya kuwa mwanakabumbu bora. Ziara hiyo ya Bolt, 32, ilipata umaarufu kote duniani. Iliongezeka hata zaidi pale alipofuma wavuni mabao mawili katika mechi ya Mariners ya kujiandaa kwa msimu mpya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |