Ligi kuu ya Uingereza (EPL) imeendelea jana, Chelsea walikuwa wenyeji wa Crystal Palace darajani Stamford na kufanikiwa kuchomoza na ushindi wa magoli 3-1. Magoli ya Chelsea yameingizwa kimiani na Alvaro Morata katika dakika ya 32 na 65, bao la tatu la Chelsea limefungwa na mhispaniola Pedro huku la kufutia machozi la Crystal Palace limepachikwa na Andros Townsend dakika ya 53.
Mchezo mwingine wa ligi hiyo ulikuwa katika uwanja wa Etihad ambapo Manchester City imefanya mauaji kwa kuifunga Southampton magoli 6-1.